Pages

Wednesday, October 17, 2012

ZANZIBAR KWA WAKA MOTO BARABARA YA DARAJANI YAFUNGWA KUFUATIA KUKAMATWA KWA KIONGOZI WA UAMSHO.


Picha na Maktaba Barabara ya Darajani Visiwani Zanzibar. Askari wa kutuliza ghasia wameshaanza kurusha mabomu ya machozi kutawanya kundi la uamsho ambao wapo Barabara ya Darajani wanachoma matairi na kurusha mawe kwa askari. Fujo hizo zimetokana na kukamatwa kwa kiongozi wa Uamsho Sheikh Farid.
Chanzo cha habari hizi ni Mdau Disminder Original kutoka Visiwani Zanzibar.
Nitaendelea kuwapa Update zaidi hapo baadae.
Huyu ndiye Kiongozi wa Kundi linaloitwa UAMSHO la Zanzibar Sheikh Farid aliyekamatwa huko Visiwani Zanzibar. Kundi hilo shughuli zake ni za mihadhara ya Kidini hasa ya Kiislam.

No comments:

Post a Comment