Test Footer

Habari Mpya

UVCCM CHAMWINO YAWATUNUKU VYETI WASICHANA WALIOPATA DARAJA LA KWANZA KIDATO CHA PILI NA KIDATO CHA NNE.

Written By peterdafi.blogspot.com on Monday, March 15, 2021 | 9:14 AM

 Chamwino:

Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Chamwino Jioni ya leo tarehe 08/03/202 1 Imetoa vyeti na vifaa vya kusomea kwa wasichana Waliofanya vyema Kidato cha Pili nacha Nne kwa kupata Daraja la Kwanza (Division one) la Ufaulu kwenye Masomo yao.
Akizungumza na Wanafunzi hao Katibu wa UVCCM Wilaya ya Chamwino Ndg Peter Dafi amewasisita Mabinti hao kusoma kwa Bidii na kuhakikisha wanaweka Historia ya kupata Msichana atakaeshinda kitaifa ambae atatoka Wilaya ya Chamwino.
Amewasisitiza kuzingatia Masomo kwa Nidhamu kwani Nidhamu ndio Msingi Mkuu wa Mafanikio ya Maisha kwa Nyanja zote.
Pia Mh Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dodoma Bi Fatma Taufiq ambae alijumuika na kuzungumza na Mabinti hao kwa njia ya simu amewasisitiza kusoma kwa Bidii na hakuna jambo linaloshindikana kama unania njema ya kufanikiwa. Pia amewatia moyo walimu wenzie na kuwaomba kuendelea kuwa na moyo wakujitoa na kuwafundisha wanafunzi bila kuchoka.



Picha ya Pamoja na Baadhi ya Wasichana waliopata Vyeti

Msichana Muwakilishi wa wenzie akitoa neno kwa niaba ya wasichana wenzie

Katibu akizungumza na Head Boy akiwa na Head Gall wa Mvumi Secondary

Picha ya Pamoja
Katibu Ndg Peter Dafi akizungumza na Vijana katika siku ya wanawake Duniani
Katibu Peter Dafi akimkabidhi Cheti cha Pongezi Msichana aliepata Ushindi wa Daraja la kwanza kidato cha Nne Mwaka jana 2020.
Katibu Peter Dafi akimkabidhi Binti alieshinda Daraja la kwanza kwenye Mtihani wa kidato cha Pili
Wanafunzi wakiimba Wimbo wa Tanzania nakupenda 
Katibu Peter Dafi akiingia ukumbini akiwa ameambatana na walimu

WARAKA No. 2 WA MHE. SPIKA KUHUSU UGONJWA WA CORONA

Written By peterdafi.blogspot.com on Tuesday, March 17, 2020 | 1:33 AM




Peter Msigwa alipiwa na Rais Magufuli.

Written By peterdafi.blogspot.com on Thursday, March 12, 2020 | 5:35 AM

Rais John Magufulileo Tarehe 12/03/2020 amemlipia Sh38 milioni Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa kati ya Sh40 milioni alizotakiwa kulipa faini baada ya kuhukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

UVCCM CHAMWINO WAJAZA FOMU KWA NIABA YA BARAZA LA WADHAMINI

Written By peterdafi.blogspot.com on Monday, March 9, 2020 | 2:56 AM

Katibu UVCCM Wilaya ya Chamwino Ndg Peter Dafi akiwa ameambatana na Mwenyekiti wake Ndg Abdallah Omar wamejaza Fomu ya Kumilikishwa Kiwanja chenye Ukubwa wa Area 10,000 SQM 25 By 40 Block D Chamwino.
Baada ya Kujaza Fomu na hapa akirudisha Fomu kwa Afisa Ardhi anaeshughulikia Mambo ya Ardhi.

MAVUNDE APOKEA MIFUKO 724 YA SARUJI KUTOKA CRDB BANK

Written By peterdafi.blogspot.com on Tuesday, July 10, 2018 | 7:08 AM

*MAVUNDE APOKEA MIFUKO 724 YA SARUJI KUTOKA CRDB BANK KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SHULE KATIKA JIMBO LA DODOMA MJINI*

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini *Mh Anthony Mavunde* leo amepokea mifuko ya Saruji 724 yenye thamani ya *Tsh 10,000,000* kutoka *Benki ya CRDB* kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa,Nyumba za Walimu na matundu ya vyoo katika shule za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Dodoma Mjini.

Akikabidhi mifuko hiyo ya Saruji,Mkurugenzi CRDB Tawi la Dodoma *Bi Rehema Hamis* amesema kwamba Benki ya CRDB inaunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya Tano chini ya *Mh Rais Dr John Pombe Magufuli* na uchapakazi wa Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde katika kuboresha miundombinu ya Elimu.

Akipokea mifuko hiyo ya saruji,Mbunge Mavunde ameishukuru benki ya CRDB kwa msaada huo ambao utalenga kupunguza changamoto ya ukosefu wa vyumba vya madarasa 1035 katika Jimbo la Dodoma Mjini ambapo kwa hivi sasa anaendesha kampeni maalum ya upatikanaji wa vifaa vya ujenzi na kwa kuanzia mfuko wa Jimbo umetoa matofali 32,000 na mifuko ya Saruji 2,560 kwa kata mbalimbali.

TANZIA: Mwanajeshi wa Tanzania auawa na wengine watano hali ni mbaya

Written By peterdafi.blogspot.com on Wednesday, June 6, 2018 | 3:31 AM


Askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya Kati Afrika wanaotokea nchini Tanzania, ameuawa na waasi huku wengine 18 wakijeruhiwa vibaya.



 Kwenye Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Ulinzi Tanzania imesema kwamba kati tukio hilo limetokea Juni 3, 2018 huko Afrika ya Kati, ambapo kikosi hiko chenye askari 90 kilishambuliwa na waasi wanaojulikana kwa jina la Sirir, na kusababisha kifo cha askari huyo mmoja, kujeruhi 18 huku watano kati yao wakiwa katika hali mbaya zaidi.
Majeruhi wa shambulio hilo wamepelekwa katika Hospitali ya Kanda ya Umoja wa Mataifa iliyopo Bangui kupatiwa matibabu, huku utaratibu wa kuurejesha mwili wa marehemu nyumbani Tanzania zikiwa zinaendelea.

MAVUNDE AWATAKA WADAU WA MICHEZO DODOMA KUSHIRIKIANA KURUDISHA HESHIMA YA DODOMA KATIKA MPIRA WA MIGUU

Written By peterdafi.blogspot.com on Sunday, June 3, 2018 | 11:18 PM

*MAVUNDE AWATAKA WADAU WA MICHEZO DODOMA KUSHIRIKIANA KURUDISHA HESHIMA YA DODOMA KATIKA MPIRA WA MIGUU*

Naibu Waziri wa Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde amewataka wadau wa Mpira wa Miguu katika mkoa wa Dodoma kushirikiana na kuweka nguvu ya pamoja ili kurudisha heshima ya Mkoa wa Dodoma katika mpira wa Miguu nchini kwa kuwa na Timu ya Ligi kuu na kuongeza hamasa kupitia mashindano ya ligi mbalimbali ili kuibua vipaji.

Mavunde ameyasema hayo leo katika kijiji cha Msanga,Wilaya cha Chamwino -Dodoma wakati akifungua mashindano ya Kombe la *Kisalazo 2018* ambalo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Ndg Juma Kisalazo na Mbunge wa Jimbo la Chilonwa Mh Joel Makanyaga Mwaka.

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger