Test Footer
WARAKA No. 2 WA MHE. SPIKA KUHUSU UGONJWA WA CORONA
Written By peterdafi.blogspot.com on Tuesday, March 17, 2020 | 1:33 AM
Peter Msigwa alipiwa na Rais Magufuli.
Written By peterdafi.blogspot.com on Thursday, March 12, 2020 | 5:35 AM
MAVUNDE APOKEA MIFUKO 724 YA SARUJI KUTOKA CRDB BANK
Written By peterdafi.blogspot.com on Tuesday, July 10, 2018 | 7:08 AM
*MAVUNDE APOKEA MIFUKO 724 YA SARUJI KUTOKA CRDB BANK KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SHULE KATIKA JIMBO LA DODOMA MJINI*
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini *Mh Anthony Mavunde* leo amepokea mifuko ya Saruji 724 yenye thamani ya *Tsh 10,000,000* kutoka *Benki ya CRDB* kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa,Nyumba za Walimu na matundu ya vyoo katika shule za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Dodoma Mjini.
Akikabidhi mifuko hiyo ya Saruji,Mkurugenzi CRDB Tawi la Dodoma *Bi Rehema Hamis* amesema kwamba Benki ya CRDB inaunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya Tano chini ya *Mh Rais Dr John Pombe Magufuli* na uchapakazi wa Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde katika kuboresha miundombinu ya Elimu.
Akipokea mifuko hiyo ya saruji,Mbunge Mavunde ameishukuru benki ya CRDB kwa msaada huo ambao utalenga kupunguza changamoto ya ukosefu wa vyumba vya madarasa 1035 katika Jimbo la Dodoma Mjini ambapo kwa hivi sasa anaendesha kampeni maalum ya upatikanaji wa vifaa vya ujenzi na kwa kuanzia mfuko wa Jimbo umetoa matofali 32,000 na mifuko ya Saruji 2,560 kwa kata mbalimbali.
MAVUNDE AWATAKA WADAU WA MICHEZO DODOMA KUSHIRIKIANA KURUDISHA HESHIMA YA DODOMA KATIKA MPIRA WA MIGUU
Written By peterdafi.blogspot.com on Sunday, June 3, 2018 | 11:18 PM
*MAVUNDE AWATAKA WADAU WA MICHEZO DODOMA KUSHIRIKIANA KURUDISHA HESHIMA YA DODOMA KATIKA MPIRA WA MIGUU*
Naibu Waziri wa Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde amewataka wadau wa Mpira wa Miguu katika mkoa wa Dodoma kushirikiana na kuweka nguvu ya pamoja ili kurudisha heshima ya Mkoa wa Dodoma katika mpira wa Miguu nchini kwa kuwa na Timu ya Ligi kuu na kuongeza hamasa kupitia mashindano ya ligi mbalimbali ili kuibua vipaji.
Mavunde ameyasema hayo leo katika kijiji cha Msanga,Wilaya cha Chamwino -Dodoma wakati akifungua mashindano ya Kombe la *Kisalazo 2018* ambalo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Ndg Juma Kisalazo na Mbunge wa Jimbo la Chilonwa Mh Joel Makanyaga Mwaka.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe Christine Mndeme , leo tarehe 3/6/2018 amekabidhiwa Mwenge wa Uhuru Na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe Christopher Ole Sendeka.
*RUVUMA NA MWENGE WA UHURU*
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma *Mhe Christine Mndeme* , leo tarehe 3/6/2018 amekabidhiwa *Mwenge* wa Uhuru Na Mkuu wa Mkoa wa Njombe *Mhe Christopher Ole Sendeka* .
Mwenge wa *Uhuru,* ukiwa Mkoani *Ruvuma* unatarajia kuzindua Jumla ya *miradi 70* yenye thamani zaidi ya Shilingi *bilioni 11.* itafunguliwa,kutembelewa na kuwekwa mawe msingi.
Mwenge wa *Uhuru* utakimbizwa Halmashauri Nane za Mkoa wa Ruvuma.
*Mwenge wa Uhuru kwa Maendeleo CHANYA ya Mkoa wa Ruvuma !*
KIFO CHA AKWILINA NI MTAJI WA SIASA KWA WANASIASA UCHWALA WA TANZANIA.
Written By peterdafi.blogspot.com on Tuesday, February 20, 2018 | 2:12 AM
Mbunge Ridhiwani Kikwete Amegawa Vifaa vya Kuchezea Mpira kwa Team ya Jimbo la Chalinze
Written By peterdafi.blogspot.com on Friday, August 11, 2017 | 2:12 PM
Mbunge wa Chalinze leo amegawa vifaa vya michezo kwa timu za jimbo la chalinze zinazoshiriki mashindano ya kombe la Mazingira linaloshirikisha timu za wilaya ya bagamoyo.
Sherehe hizo zilizofanyika kimange zilihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo Madiwani wote wa Jimbo la Chalinze na watendaji wao wa kata ambao walipokea jezi kwa niaba ya timu zao. Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ambaye ndiye muandaaji mkuu wa mashindano hayo akishirikiana na wabunge wa majimbo yote
Pamoja na kugawa jezi , mbunge wa chalinze aliwaahidi kuwapatia mshindi wa pili wa mashindano Pilkipiki ya Miguu miwili, na jezi kwa timu zote Tatu za juu kufuatia mkuu wa wilaya kuwachangia mshindi wa kwanza pikipiki ya Toyo ya miguu mitatu ili itumike kwa shughuli za kipato kwa vijana.
MAISHA YA MAZOEA CCM IFIKIE KIKOMO ~ HAPA KAZI TU!
Written By peterdafi.blogspot.com on Saturday, July 9, 2016 | 11:23 AM
MAISHA YA MAZOEA CCM IFIKIE KIKOMO ~ HAPA KAZI TU!
Nasema hivi.....!
Hakuna Kipindi ambacho wana CCM wanatakiwa kuwa Makini na siasa kama Kipindi hiki.
Hakuna Kipindi wana CCM wanatakiwa Kuacha Tabia zakimazoea km kipindi hiki.
Hakuna Kipindi ambacho chama na jumuiya zake kinapaswa kuajiri Vijana na Watu wenye Uwezo Mkubwa wakufikiria nakupanga mikakati ya Kisasa inayokwenda na Wakati kama Kipindi hiki.
Tunaposema vijana.... Umri siyo tija ingawa ni Jambo la maana kwa Mustakabali wa taifa na Chama.... Bali tunahitaji vijana wanaoweza kuunganisha kasi yao ya mwendo huku wakitumia busara na hekima wanazochota kutoka kwa wazee na waasisi wetu.... Sifa siyo Umri, Sifa iwe ni uwezo wa kutenda na kufanya, kuona na kuangalia, kusikia na kusikiliza na kufanya kuyafanyia kazi yote kwa pamoja...... Huyo ndiye kijana apewe nafasi......
Hakuna Kipindi ambacho hatutakiwi kuishi kwa UWoga, Unafiki, Uzandiki km kipindi hiki, tunapaswa kuwa wawazi ili kujua tatizo liko wapi.
Tabia za kufanya Ziara nakufika Mikoani uko, Katibu anatoa Takwimu za Uwongo za uwingi wa Wanachama ama utendaji kazi zake wakati hazina ukweli na anahali ngumu na Tete yakisiasa ktk eneo lake ikome.
Tunapaswa kufanya Kazi kubwa ya Siasa kwa umakini ili Chama kiwe imara na Serikali iwe Imara na Hatimae Ilani ya CCM itimizwe kwani nilazima tuwe shupavu ili itekelezeke kwa 99% kwani CCM ndio Chama Tawala na CCM ndio yajenga Nchi.
Kwani Mafanikio na Mipango chanya itakayotekelezeka ndio haswaa itajenga mizizi imara itakayoifikisha CCM Miaka 50+ ijayo.
Swala la Uwanachama nilazima sasa tuhakikishe Wanachama wa CCM wanafanyiwa Vetting na Mafunzo yakikada kama huko awali ilivyokuwa lazima Mwanachama apitie mafunzo miezi 3 tujiridhishe kuwa kafuzu na yuko sawa ki Itikadi "NILAZIMA TUWE NA WANACHAMA WA ITIKADI NA SIO WANACHAMA WA KADI" hawa wanachama wa Kadi ndio wanaotuyumbisha leo CCM kesho NCCR na Tulimuamini tukampa cheo bila kujua Ulaji ndio ulimleta CCM.
Wakirudisha Kadi za Vyama CDM na Vyama Pinzani vingine Basi Tutawapokea kisha Watakaa kupewa Darasa la Itikadi kwa Miezi 3 ili Tujiridhishe kuwa Anania na amekwiva.
Pia nikuhakikisha tuna Team inayochunguza Mienendo ya Wanachama hawa na tena iwe Fear isije ikasema uwongo.
Tunahitaji Mabadiliko ya Kweli kama tulivyoimba Katika Kampeni.
Naamini Kuwa Tunapoelekea Kumkabidhi M/kiti Mpya Chama basi Haya yawe ni Vipaumbele pia vya Mambo yakushughulikiwa ndani ya Chama.
Naitwa Peter Dafi
Mtetezi wa Wanyonge.
09/07/2016
VILAZA WA UKAWA ACHENI USONGOMBWINGO
Written By peterdafi.blogspot.com on Friday, July 8, 2016 | 8:33 AM
Acheni unazi bana
Peter Dafi
Mkuu wa Wilaya Ally Salum Hapi Akabidhiwa Fimbo yakuchapia Mafisadi na Wazee wa IKICHE
Written By peterdafi.blogspot.com on Sunday, May 8, 2016 | 3:09 AM
Mh DC wa Kinondoni Ally Salum Hapi awa mgeni Rasmi katika kikundi ambacho kina wanachama 76 kati yao hao Wanaume ni 36 na Wanawake ni 40.
IKICHE ni kikundi ambacho kinafanya shughuli za kukopeshana kwa Shida na Raha.
Kikundi kina Miaka Minane Leo hii na kimedhaminiwa Cheti cha Usajili, Kikundi cha IKICHE kilianzishwa 13/04/2008 Jijini Dar es salaam

DC HAPI ATEMBELEA GHAFLA HOSPITALI YA MWANANYAMALA USIKU LEO
Written By peterdafi.blogspot.com on Wednesday, May 4, 2016 | 2:52 PM
DC HAPI ATEMBELEA GHAFLA HOSPITALI YA MWANANYAMALA USIKU LEO
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Salum Hapi leo usiku ametembelea hospitali ya Mwananyamala kujionea utoaji wa huduma hasa wakati wa usiku.
Hapi ambaye alitinga hospitali hapo kama mgonjwa wa kawaida akivalia kofia ya mkeka alitembelea mapokezi, vyumba vya daktari na baadae kumshtukiza kiongozi wa madaktari kwa usiku huo ofisini kwake akimuelekeza kumtembeza sehemu mbalimbali za hospitali hiyo ambayo Mkuu wa wilaya alitaka kuziona.
Mh. Hapi alitembelea wodi ya watoto, wanaume, wodi ya kina mama, wodi ya dharura (emergency) na kumalizia chumba cha kuhifadhia maiti (mortuary) ambako alizungumza na wagonjwa, kuwajulia hali na kujionea changamoto zinazowakabili.
Akiwa chumba cha kuhifadhia maiti Mh. Hapi alifanya mazungumzo na mhifadhi maiti na kujua changamoto zinazoikabili ofisi yake.
Hospitali ya Mwananyamala inatajwa kuwa na changamoto nyingi za utoaji huduma hali inayosababisha malalamiko ya mara kwa mara ya wananchi.






