Home » , » Mgomo wa AngloGold Ashanti waenea Afrika Kusini

Mgomo wa AngloGold Ashanti waenea Afrika Kusini

Written By peterdafi.blogspot.com on Thursday, September 27, 2012 | 1:24 AM



Mgomo uliokumba mojawapo ya migodi nchini Afrika Kusini wa dhahabu ,AngloGold Ashanti, sasa umeenea hadi katika migodi mingine ya kampuni hiyo nchini humo.
AngloGold imesema kuwa wengi wa wafanyakazi wake, takriban 35,000 nchini humo, wanashiriki katika migomo hiyo wakidai nyongeza ya mishahara.
Mgomo huu unajiri baada ya wafanyakazi wa kampuni ya madini ya Lonmin kurejea kazini wiki jana baada ya kugoma vile vile wakitaka mishahara mizuri.
Takriban watu 46 waliuawa wakati wa maandamano ya kudai nyongeza ya mishahara katika mgodi wa Marikana.
Uchunguzi wa mauaji hayo utaanza tarehe moja mwezi ujao.
Mgomo mwingine ambao hauhusiani na huu wa AngloGold, unaendelea katika mgodi mwingine wa dhahabu wa Gold Fields.
Mgomo huu wa AngloGold ulianza wiki jana katika mgodi wa Kopanang na kuenea hadi katika mgodi wa Mponeng ambao ndio wenye uketo mkubwa zaidi duniani.

Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger