Home » »

Written By peterdafi.blogspot.com on Thursday, September 20, 2012 | 2:46 AM



Wapenzi wa filamu za marehemu Steven Kanumba watakuwa na uhakika wa kumuona tena staa huyo aliyefariki April mwaka huu kwenye filamu mpya.

Filamu hiyo inaitwa Ndoa Yangu ambapo Kanumba aliigiza na Jackline Wolper.

Ndoa Yangu inatarajiwa kuingia sokoni September 28 ikiwa chini ya usambazaji wa kampuni Steps Entertainment.

Tangu kifo cha Kanumba, hiyo itakuwa ni filamu yake ya kwanza kutoka huku kampuni ya Steps ikidai kuwa imetengenezwa kwa kiwango cha juu na pia haiwezi kukopiwa kirahisi na maharamia kutokana na kutumia teknolojia ya ufungaji filamu.
UNA MTAZAMO GANI JUU YA HABARI HII? TUPE MAONI YAKO
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger