Home » » BASHE CHUPUCHUPU KUTEKWA.....!.

BASHE CHUPUCHUPU KUTEKWA.....!.

Written By peterdafi.blogspot.com on Thursday, April 4, 2013 | 2:26 AM




WIMBI la viongozi wakuu wa

Kampuni ya New Habari (2006)

Ltd, kuendelea kuwindwa na

watu wasiofahamika,l imeendelea

kushika kasi baada

ya usiku wa kumkia jana,Ofisa

Mtendaji Mkuu wa kampuni

hiyo,Hussein Bashe kunusurika

kutekwa.Tukio hilo lilitokea juzi

usiku wakati Bashe alipokuwa

akitoka ofisini kwake Sinza

Kijiweni, akielekea nyumbani

kwake Mbezi.


Akizungumzia tukio hilo, Bashe

alisema wakati anaondoka

ofisini kwake kwa gari lake,

alianza kufuatiliwa kwa nyuma

na magari mawili, likiwamo aina

ya NOA ambalo hata hivyo

hakufanikiwa kujua lilikuwa na

watu wangapi.


“Kama kawaida nilishinda ofisini

kwa ajili ya majukumu yangu ya

kazi na muda wa kutoka

ulipowadia, niliondoka kurudi

nyumbani.


“Awali wakati navuka geti la pale

ofisini,sikuwa na shaka yoyote,

lakini kadri nilivyozidi kuendelea

na safari yangu, niliona nyuma

nafuatiliwa na magari mawili

ambayo yalikuwa yakiendeshwa

kwa tahadhari.


“Nilipofika Mwenge ile NOA

ilikuwa bado iko nyuma yangu,

sasa nikaanza kupatwa na

wasiwasi, nikajua hapa kuna

jambo.

“Moyoni niliendelea kumuomba

Mungu, huku nikijiuliza maswali

mengi hawa jamaa ni akina nani,

kwa kweli sikupata jibu zuri.


“Nilipofika Mbezi, niliona yale

magari yanazidi kunisogelea,

kwa hiyo,nikaamua kuongeza

kasi na wao wakazidi kuja tu.

“Wakati niko Mbezi jirani na njia

panda ya kwenda kwangu,gari

moja lilinipita kwa kasi na

kuendelea mbele.

“Unajua kuelekea kwangu pale

kuna barabara kama tatu

ambazo zote unaweza kuzitumia

na zikakufikisha hadi nyumbani

kwangu,”.

Alisema Bashe na

kuongeza:

“Nilichokifanya nilipita barabara

ya kwanza na wao wakapita

barabara ya pili na ghafla

nilikutana nao uso kwa uso,

wakati huo naelekea kwangu na

kibaya zaidi,gari lao walizima

taa kubwa na kuacha ndogo.

“Walivyona gari langu,walinipiga

taa kuashiria wanakata kona,

lakini cha ajabu walinifuata

nyuma na hapo nikaanza kujua

sasa nafuatiliwa.


“Nilichokifanya sikwenda

nyumbani moja kwa moja,bali

niliamua kupaki gari kwenye

grosari moja iliyoko jirani na

kwangu.


“Baadaye niliamua kuondoka ili

niwazunguke kwa nyuma

nisome namba za gari lao,lakini

sikufanikiwa kwa sababu taa za

nyuma zilikuwa zimezimwa,”

alisema Bashe.


Kwa mujibu wa Bashe,baadaye

aliingia nyumbani kwake na

kuwakuta wageni ambao alikaa

nao hadi saa sita usiku baada ya

kuwasimulia tukio lilivyokuwa.


“Sasa basi, wakati jamaa zangu

hao wanaondoka kurudi kwao,

walikuta lile gari pale pale njiani,

wakanipigia simu, kwamba lile

gari nililowasimulia

linawafuatilia.

“Nikawaambia wageuze gari lao

ili wasome namba, lakini

hawakufanikiwa hata kidogo

kwa sababu wale jamaa

walishtuka na kuamua kutimua.


“Kwa hiyo, nilichokifanya

nilikwenda pale Polisi Kawe na

kutoa taarifa ambapo nilipewa

RB yenye namba KW/

RB/2899/2013,” Alisema.


Machi 6, mwaka huu, Mhariri

Mtendaji Mkuu wa New Habari

(2006) Ltd, Absalom Kibanda,

alitekwa na kuteswa na watu

wasiofahamika.

Katika tukio hilo, Kibanda

alitobolewa jicho la kushoto,

alipigwa kichwani na kitu

chenye ncha kali na kunyofolewa

kucha.Kwa sasa yuko nchini

Afrika Kusini ambako anaendelea

na matibabu.


SOURCE:

MTANZANIA.

2013 March 30.
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger