Home » , » FUATILIA SAKATA LA KUBAKA LA MBASHA MUME WA FROLA MBASHA HAPA......!!

FUATILIA SAKATA LA KUBAKA LA MBASHA MUME WA FROLA MBASHA HAPA......!!

Written By peterdafi.blogspot.com on Sunday, June 8, 2014 | 5:21 AM

NIKO KAWE HAPA NASIKIA FROLA MBAYA ANAIMBA WIMBO WA JIPE MOYO........
KANISANI KWA GWAJIMA.....!!
Emmanueli Mbasha akiwa na Mkewe Flora Mbasha Pichani

Naomba nifunguke kidogo nielezee kile ninachokifahamu kuhusu ili sakata!! Mgogoro katika ndoa ya Mbasha na Florah ulianza kushika kasi mwaka jana mara baada ya Florah na Mumewe kuhamia kuanza kusali kanisani kwa GWAJIMA (ufufuo na Uzima - kawe) wakitokea kanisa la MITO YA BARAKA (kariakoo)! Inasemekana kuwa mara baada ya kuhamia kanisani hapo kwa mualiko wa Gwajima (aliwaombe waje kusali kwake), mchungaji Gwajima alimfanya florah kama kiongozi wa Ibada ya SIFA na KUABUDU katika mikutani yake!! Kama ni mfuatiliaji wa haya mambo utakumbuka kuwa mwaka jana Florah alizunguka Tanzania nzima akiwa na Gwajima wakifanya mikutano ya Injili!! Baada ya Muda kidogo Mchungaji Gwajima alimpeleka Florah London kwaajili ya masomo kitendo ambacho inasemekana kilipingwa sana na mumewe Mbasha! Ikumbukwe kuwa GWAJIMA haiwezi kupita miezi miwili pasipo kwenda UK coz amefungua kanisa kule (GLORY OF CHRIST - UK)!! So katika kipindi ambacho florah alikuwa London walikuwa wanaonana mara nyingi sana na GWAJIMA... Baada ya Florah kurudi Tanzania ndipo akaanza hii ziara ya kuzunguka mikoani na GWAJIMA.. inasemekana kuwa katika kipindi hiki ndipo mahusiano ya kindoa kati ya forah na mumewe yalizorota zaidi... baada ya ziara kuisha Florah arirudi nyumbani lakini she wasn't the same (nisiseme zaidi)! Baada ya mikwaruzano ya hapa na pale ndipo Florah akaenda kukaa hotelini na inasemekana hoteli ilikuwa inalipiwa na mchungaji GWAJIMA, ikumbukwe kuwa ni swala la kawaida kwa Gwajima kuwalipia bills mbalimbali viongozi wake wa huduma hapo kanisani kwa mfano anamchngaji anaitwa MAXMILLIAN MACHUM amempangishia nyumba ya ghorofa pale ubungo na wachungaji wake wote wapatao thelethini amewanunulia magari!! Lakini hata hivyo hii hatua yake ya kumpangia hoteli mke wa mtu ilizua maswali mengi sana..... NAOMBA TUDIGEST HII KWANZA ALAFU NTARUDI HAPA KUELEZEA YAFUATAYO 1. Kisa cha mbasha “kubaka" 2. Milioni 10 alizotoa GWAJIMA kwenye msiba wa kulola 3. Mungu akinipa ujasiri nitamtaja kabisa mtu aliye nyuma ya pazia ya hii sinema.. ----------------------------------------- 

 By The bold Iko hivi wakuu.. 1. Kisa cha mbasha “kubaka" (Sitatoa kila detail ili kulinda identity yangu) Kabla sijaanza kueleza kisa hiki ni vizuri niwaeleze kidogo kuhusu Intellijensia ya Gwajima jinsi ilivyo... pale kanisani kwake wanavitengo mbali mbali amabvyo wenyewe wanaviita ‘ministries' na katika ministry hizo zipo mbili ambazo ni muhimu zaidi i) Media ministry ii) Security ministry (hii huwa wanaiita ‘mashujaa' wa Daudi)... Media - Ministry kazi yake ni kulitangaza kanisa mitaani na kwenye vyombo vya habari, kueneza ‘propaganda' ya kanisa na mambo mengine yanayofanana na hayo. Security Ministry - kazi yao ni kumlinda Gwajima.! Kama umewahi kufika pale kanisani utakuwa umewahi kuwaona huwa wanavaa suti nyeusi na miwani nyeusi (kama secret service wa marekani).. wale jamaa usiwachukulie poa, majamaa wale ni wanajeshi na polisi wastaafu na wengine bado wapo kazini.. Sasa huduma hizi mbili zinaunda kitu kama “USALAMA WA TAIFA" wa kanisa la Gwajima.. Turudi kwenye topic sasa.... Ni ukweli ambao ulikuja kubainika hivi karibuni kuwa Mr. Mbasha ana mahusiano ya kimapenzi na shemeji yake (kwa muda mrefu kidogo) na habari hii ikamfikia mpaka florah.. kipindi hiki florah bado anakaa hoteli! Suala hili florah aliwaeleza watu wachache sana wakaribu na likabakia kuwa siri.. lakini sisi wengine tikuwa tunalifahamu muda mrefu tu! Kuna watu wakamshauri florah amuhoji mmewake na florah akauchukua huo ushauri akaenda kumuhoji Mr. Unaambiwa jamaa aling'aka balaa na akakataa kata kata kuwa hana mahusiano na shemejiye! Basi katika majibizano mara jamaa akaropoka kuwa mbona hata yeye anafahamu kuwa florah anamahusiano na Gwa**** lakini hasemi chochote! Weeeeee ilikuwa balaa maana hicho kilikuwa kijikikao fulani hivi na ndugu kadhaa walikuwepo basi kila mtu akashikwa na bumbuwazi!!! Unaambiwa flaorah hakusema chochote akaanza kulia akainuka akaondoka!! Na baada ya hapo hata simu za mbasha akawa hapokei... Inasemekana taarifa zikamfikia mchungaji wao Gwajima, basi Gwajima akamuita ofisini jamaa akakataa kwenda! Sasa katika hizo purukushani za kuwasuluhisha jamaa kuna siku akatishia kuwa atavujisha ushahidi wa mahusiano ya huyo mchungaji na mkewe florah!! Nahisi hapo ndipo alipojiroga.. KESI YA KUBAKA baada ya mrafaruku kutokea jamaa akawa dizaini kama amesitisha mahusiano na shemejiye na hapa kati alikuwa hakai nyumbni kwa florah.. lakini inavyoonekana mchungaji alitishwa sana na mkwara wa jamaa kuwa atavujisha ushahidi wa mahusiano yake na mkewe... binafsi nahisi mipango ikaanza kusukwa na binti akasetiwa kwa ajili ya ‘operation tokomeza'!! Juzi juzi hapa kabla ya tukio kutokea ndio huyu binti amerudi kwa florah akijua wazi kabisa dada take hayupo! Na kama ujuavyo muonja asali aonji Mara moja, jamaa kuona mzigo umerudi basi ikabidi wakumbushie enzi! Sitaki kumaliza huondo wote lakini tujiulize maswali haya!!! 1. Hivi kubaka ndio inakuwa hivi? Ni ijumaa mko nyumbani peke mnamaliza kula mchana mnakaa sebuleni mnapiga stori ‘mizuka inapanda mnaamua kuibanjua amri ya sita! Kesho yake jumamosi anakuja mgeni mnakuwa wapole tu, mnavunga mnaitana shemeji! Alafu kesho kesho yake jpili mnatengeneza mazingira ili muondoke peke yenu wawili! Mnafika mahali fulani ubungo mnapaki gari mafichoni mnaanza kuibanjua amri ya sita! Mnatoka hapo mnaenda kanisani mnatabasamu kabisa, ibada ikiisha mnatengeneza tena mazingira ili muondoke peke yenu! Mnafika kisehemu chenu mnapaki tena gari mnabanjuka! Halafu eti amebakwa??????? Swali la pili la kilujiuliza! Kwanini huyu binti baada ya tukio kutokea akawapigia simu bodyguards wa Gwajima ambao walienda kumchukua na kurudi nae nyumbani kwa gwajima??? Alafu eti hawa bodyguards ndio wanaanza kuwapa taarifa ndugu za florah!! Kwanini apige simu kule?? Kwanini hakuwapigia simu ndugu zake kwanza????? By The bold Swali la tatu... Kwanini hii ishu wameipeleka fasta kwenye media! Yani binti yuko polisi anaandika maelezo wao wameshawapigia simu waandishi wako nje wanawasubiri kumuhoji! Binadamu huwa wepesi kutangaza habari njema zinazotuletea sifa! Inakuwaje habari mbaya na kudhalilisha familia kama habari hii wao wanakuwa wepesi kiasi hicho kuipeleka kwenye media??? Alafu kama hiyo haitoshi wanamrekodi mbasha na kuivujisha audio kwa makusudi kabisa ili iweje!! Kama kweli jamaa amebaka mbona wanatapatapa kutafuta huruma ya wananchi na media??? Kwanini wabehave namna hii???? ----------------------------------------------------- 
Huyu ndo Emmanuel Mbasha anakabiliwa na Kesi ya Kumbaka Shemeji yake

By The bold Jamani sitaki kumtaja mtu jina naomba mjiongeze wenyewe! Mtu akitaja jina mie simo Ila kwa kifupi hapa namuongelea mchungaji mmoja maarufu sana hapa town, anasukuma ndinga ya maana (hummer), ana mjengo wa maana wa ghorofa nne mbezi beach, na ana hela mpaka hajui azifanyie nini, ana mtoto wa kike anasoma high school nchini Switzerland, na juzi juzi amenunua magari 32 yenye jumla ya thamani ya zaidi ya milioni 250 ameyagawa kwa wasaidizi wake kanisani kwake! USHIRIKI WAKE KWENYE BIASHARA YA SEMBE. Huyu mtumishi ana dada zake wawili wote wameolewa na wachungaji wake wasaidizi hapo kanisani kwake, mmoja anaishi ubungo mwingine anishi kibaha kwa Mathias.! Hapa nataka kumuongelea huyo anayeishi kibaha kwa Mathias, yeye na mme wake wamejaliwa kupata watoto wawili, na mumewe ni Kiongozi kanisani kwao (kanisani kwa kaka yake) upande wa ulinzi na usalama.. na anahusika moja kwa moja na ulinzi wa mchungaji wetu tunayemuongelea hapa (mzee wa humer na misukule)! Kwa kifupi jamaa yuko katika ‘inner circle' ya mzee wa hummer na misukule! Sasa huyu jamaa (shemeji/mlinzi wa mzee wa Hummer) mwaka jana alimleta binti kutoka kijijini kwao akasema kuwa ni mtoto wa shangazi yake!! Baada ya miezi kadhaa mkewe akagundua kuwa jamaa anammega yule binti, basi kukawa na ugomvi mkubwa sana, mpaka mzee wa hummer ikabidi aingilie!! Baada ya kuingilia na kumtetea dada yake, shemeji mtu akamaindi sana kiasi ambacho akaacha hata kwenda kusali kule kanisani na mpaka cheo chake cha chief security officer wa mzee wa hummer akakipiga chini! (Huyu jamaa ni mwanajeshi kikosi cha hapa kigamboni) Kupitia huyu bwana ndio tukanyetishwa hili suala ntalolielezea hapa.. Mwaka jana mwezi novemba kuna gazeti moja la global liliandika habari kuwa mzee wa hummer amelishwa sumu na askofu watu wakaponda kuwa ni uongo ila mzee wa hummer anataka kujipa promo! Ile ishu ilikuwa ni kweli coz hata mimi mwenyewe niliifahamu karibia miezi minne kabla haijatoka kwenye gazeti ila nilikuwa sikujua why askofu alimlisha sumu, na sababu ambayo baadae global waliitoa ilikuwa ya kijinga mno eti jamaa wenzake wanamuonea wivu! Sasa huyu mnyetishaji wangu ndo amenifumbua macho.. ishu iko hivi!! Jamaa anasema kuwa katika sekta ya hawa ‘watumishi wa mungu' kuna CARTEL ya watu sita ikiwajumuisha mzee wa hummer, mchungaji mmoja wa kike ana kanisa mikocheni B pamoja na mwingine ana kanisa kubwa sana Mwenge (sio kakobe) huyu anajiita ‘mtume na nabii'! Anaendelea kusema kuwa hawa wawili (mama wa mikocheni na mtume wa mwenge) wao ni wazoefu sana lakini huyu mzee wa hummer ni wa juzi tu kwenye mtandao ila ni mjanja mni coz ameweza kujenga mtandao mpana sana na amekuwa akiwazunguka wenzie! Sasa anadai kuwa mwaka jana ugomvi wao ulifikia pabaya zaidi kiasi kwamba wenzie walidhamiria hasa kumuua!! Mwaka jana pekee mzee wa hummer alivamiwa mara mbili nyumbani kwake na watu wasiojulikana na hawakuiba chochote inasemekana kuwa walikuwa wanamsaka mzee wa hummer bahati nzuri hakuwepo (hili Mimi mwenyewe binafsi nimelithibitisha kupitia kwa ndugu zake wa karibu) (Mwishoni ntaeleza connection iliyopo na tukio la Mbasha) Itaendelea... ----------------------------------------------- 

By The bold Tunaendelea wakuu... Baada ya mbinu ya kuvamia nyumbani kwa mzee wa hummer kufeli, washirika wenzie wa sembe (mama wa mikocheni na mtume wa mwenge) walijaribu kumvamia mzee wa hummer akiwa anaelekea kigoma (kigoma ndio kanisa la pili kwa ukubwa la mzee wa hummer baada ya hili la dar) lakini pia nayo kumbe aliwawekea kanyaboya mwenyewe alikwea pipa hummer alikuwa anaendesha mchungaji wake msaidizi! Baada ya mbinu zote hizi kufeli ndipo mama wa mikocheni na mtume wa mwenge wakambembeleza sana jamaa kuwa wafanye kikao wasuluishe na waangalie namna gani watasonga mbele na biashara! Basi kikao kikapangwa kifanyike alhamisi nyumbani kwa Mtume wa mwenge! Mzee wa hummer akakubali.. Siku ya alhamisi ilipofika mzee wa hummer akaenda hadi nyumbani kwa mtume, akamkuta na mama wa mikocheni amefika! Sasa sijui wakafanya sarakasi gani ndio wakampatia kinywaji chenye sumu... baada hali kubadilika ghafla mzee wa hummer ikabidi arudi home!! Afu jamaa akawa hataki kwenda hospitali, nakumbuka ilibidi mpaka dada yake mkubwa aitwe.. na daktari wake nae akaitwa! Basi jamaa akapigwa sindano ya usingizi akapelekwa kwenye zahanati ya huyo dokta mbezi beach!! Ilibidi mpaka afanyiwe upasuaji coz walisema sumu aliyokula inasababisha organs ziharibike, nakumbuka walimpasua wakakata sehemu fulani ambayo walidai kuwa imeanza kuharibika!! Kama unakumbuka vizuri mwaka jana kuna kipindi karibia miezi mitatu jamaa alikuwa haonekani wakatangaza kuwa yuko nje kwenye ziara anahubiri... jamaa alikuwa kwake paleplae anuguza mshono.! Baada ya mshono kupona jamaa inasemekana ikabidi aanze network ya kusukuma sembe pasipo kutegemea ile CARTEL yao ya watu sita! Nakumbuka alifanya vitu vitatu.. 1. Alileta wakorea saba, anaishi nao nyumbani kwake mpaka leo!! Huwa wanajifanyaga wapiga vyombo pale kabisani but wanakazi maalum ntaieleza baadae! (Hawa hata ukienda sasa hivi unawakuta) 2. Akafanya recruitment ya kufa mtu! Hapo ndio wakaingizwa dada yetu muimbaji na mmewe, akina mkandamizaji waliponea chupuchupu... baada ya mda mfupi kama mnakumbuka dada yetu akapelekwa UK (eti kusoma) (ntakuja kueleza aliwahitaji kwa nini na kilitokea nini) 3. Kuna wachungaji wake wapatao kumi na saba wakapelekwa nje (Asia na London) kwa excuse mbalimbali (kusoma na kusimamia makanisa(sijui makanisa gani)) Sasa hapa ndipo kwenye uhondo, coz kuna series of events zilitokea mpaka zikaja kuzaa hii scandal ya mume wa dada yetu muimbaji kubaka.. Ntarudi..

Chanzo:- JF 




Huyu ndo Sheji wa Mbasha anaesadikika kuwa alibakwa na sheji yake Mume wa Dada yake


Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger