Home » , , » Watu wa Benghazi wataka amani

Watu wa Benghazi wataka amani

Written By peterdafi.blogspot.com on Sunday, September 23, 2012 | 5:21 AM


Maandamano ya kupinga wapiganaji mjini Benghazi
Waandamanaji waliisihi serikali ya Libya iyapige marufuku makundi ya wapiganaji ambao wamekataa kukabidhi silaha zao tangu vita dhidi ya Kanali Gaddafi mwaka jana.
Waandamanaji wanataka serikali izidishe jeshi na polisi, na walimsifu balozi wa Marekani aliyeuliwa mjini humo juma lilopita.
Waliimba wakati wakiandamana kuelekea medani kuu ya Benghazi.
Muandamanaji mmoja, Faisla al-Naas, alieleza sababu zao:
"Sisi tunaandamana kupinga kundi lenye silaha ambalo halidhibitiwi na serikali.
Wapiganaji hawa wanafaa kujiunga na serikali ili watu wakae kwa salama.
Nchi yetu imekuwa na mtafaruku."
Maandamano mengine ya kuunga mkono wapiganaji yalikuwa madogo sana.
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger