Home » » Arsenal wafunga 2-0 lakini watolewa.

Arsenal wafunga 2-0 lakini watolewa.

Written By peterdafi.blogspot.com on Wednesday, March 13, 2013 | 9:06 PM



Olivier Giroud afunga bao
Licha ya kuifunga Bayern Munich ya Ujerumani mabao mawili kwa bila ugenini, Arsenal waondolewa katika mashindano ya Klabu bingwa bara Ulaya.
Hii ni kwa sababu katika mechi ya awali iliyochezwa wiki mbili zilizopita katika Uwanja wa Emirates, Arsenal walifungwa magoli 3-1 na Bayern.
Mchezaji Olivier Giroud aliipatia 'The Gunners' goli lao la kwanza katika dakika ya 15 baada ya pasi safi kutoka kwa Theo Walcott.
Kufuatia bao hilo Arsenal wakawa wanahitaji magolo mengine mawili ili kumaliza mechi wakuwa juu kwa 3-0.
Mlinda lango wa Arsenal Lukasz Fabianski alifanya kazi ya ziada kwani alipangua mikwaju kadhaa kutoka kwa mshambulizi matata Arjen Robben hivyo kumnyima nafasi ya kuifungia Bayern Munich goli lolote.
Lakini baada ya mechi , Bayern Munich ndio walifaulu kuingia hatua ya robo fainali.
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger