Inawezekana hili likawa moja kati ya maswali uliyonayo na hujawahi
kupata nafasi ya kumuuliza muhusika au inawezekana ikawa ni ishu ambayo
umewahi kuisikia au kuisoma kwenye chombo chochote cha habari.
Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete ambae ni mtoto wa Rais wa Jamuhuri
ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete kwenye exclusive interview na
millardayo.com anasema >>> ‘kuwa mtoto wa Rais changamoto kubwa
ambayo nimeiona mojawapo ni watu kukupa tafsiri ya vitu vingine ambavyo
wewe huvijui, kumekua na malalamiko mengi sana kwamba huyu jamaa ana
mali hizi na hizi’
‘Wanasema kampuni za mafuta, Oil Com, Camel Oil na Lake Oil ni za
kwangu, sasa unajiuliza huyo mtu ambae anaweza akatengeneza kampuni tatu
zinazofanya shughuli moja kwa nini asianzishe kampuni moja ikawa kubwa
zaidi ?? kwa hiyo kumekua na manenomaneno mengi, hizo ni changamoto
mfano kwenye siasa huku, watu wengi aidha hawajui nimetokea wapi au
wanajitoa akili katika maana kwamba hawataki kujua nimetoka wapi’
Ridhiwani Kikwete ajibu Tuhumu zake Dhidi ya Vituo vyama Mafuta nk....!!
Written By peterdafi.blogspot.com on Wednesday, June 18, 2014 | 2:14 AM
Related Articles
- Mbunge Ridhiwani Kikwete Amegawa Vifaa vya Kuchezea Mpira kwa Team ya Jimbo la Chalinze
- MAISHA YA MAZOEA CCM IFIKIE KIKOMO ~ HAPA KAZI TU!
- WARAKA No. 2 WA MHE. SPIKA KUHUSU UGONJWA WA CORONA
- UVCCM CHAMWINO WAJAZA FOMU KWA NIABA YA BARAZA LA WADHAMINI
- MAVUNDE APOKEA MIFUKO 724 YA SARUJI KUTOKA CRDB BANK
- TANZIA: Mwanajeshi wa Tanzania auawa na wengine watano hali ni mbaya
Post a Comment