Home » » Mkutano wa mapitio wa Mpango wa Taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele wazinduliwa jijini Arusha

Mkutano wa mapitio wa Mpango wa Taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele wazinduliwa jijini Arusha

Written By peterdafi.blogspot.com on Wednesday, June 1, 2016 | 2:58 AM


Mkutano wa mapitio wa Mpango wa Taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele wazinduliwa jijini Arusha
 

Picha ya pamoja ya mgeni rasmi akiwa na watumishi toka wizara ya afya,waratibu wa halmashauri na wadau toka mataifa mbalimbali


Waratibu wa mpango huo kutoka halmashauri mbalimbali wakijiandaa Kuwasilisha mada jinsi walivyofanikiwa kutekeleza mipango hiyo kwa mwaka 2015/2016,wa kwanza kulia ni dkt.Mabai Leonard(Mwanza) katikati dkt.Faraja Lyamuya(Dodoma) na dkt.Ida Ngowi(Ruvuma)

Prof.Magimba akifungua mkutano wa 5 wa mapitio wa Mpango wa Taifa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ambao unapitia na kupanga mikakati ya utekelezaji wa kutoa elimu,kukinga na kutibu magonjwa hayo nchini ambayo ni usubi,vikope(trakoma),kichocho,minyoo ya tumbo pamoja na matende na mabusha


Baadhi ya wadau wa mpango wa taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele toka nchi mbalimbali wakichangia mada kwenye mkutano huo

Prof.Magimba mwenye tai nyekundu(aliyekaa katikati)akiwa kwenye picha ya pamoja wadau wa maendeleo toka mashirika mbalimbali toka tanzania na nje ya nchi

Mgeni rasmi wa mkutano huo Prof.Ayoub Magimba(Kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR)Dkt.Mwele Malecela(kulia)katikati ni Mratibu wa mpango huo dkt.Upendo Mwingira

Prof.Ayoub Magimba akisalimiana mshauri wa kitaalam wa shirika la RTI international toka Washington DC


Prof.Magimba akiwa pamoja na watumishi wa wizara ya  afya na wa mpango wa Taifa wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchini


Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger