Home » » ZITTO NA VIBARAKA WENZIO ACHENI SIASA TU

ZITTO NA VIBARAKA WENZIO ACHENI SIASA TU

Written By peterdafi.blogspot.com on Wednesday, June 8, 2016 | 12:52 AM

ZITTO NA VIBARAKA WENZIO ACHENI SIASA TU!

Kwa Kifupi tu..... !

Zitto na wanasiasa wengine mnatakiwa kushtakiwa na kufungwa jela.....
Ikiwa watanzania wa majimbo yenu waliwachagua ili muwatumikie mkiwa bungeni, nyie mumekuwa watovu wa nidhamu mpaka kufukuzwa Bunge, hebu Zitto tuambie, una uhalali gani wa kuendelea kukaa uraiani???? Kwa nini usijipeleke jela????

Nasimamia ibara ya 27(2) wajibu wa kila raia kuilinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania..... Iweje mumeshindwa kukaa bungeni, mnakuja kupotosha Umma.....????

Uzuri Tanzania tunalo jeshi makini na lenye weledi, limekumbuka kuwazuia nyie wapiga siasa uchwara msisumbue watu walioko kazini....

Hivi Zitto, kwa nini usiridhike kwamba siasa zako zimepita wakati wake????? Kwa nini usikubali kwamba muda wa kuendelea kuhadaa Umma umekwisha???? Kwa nini usikubali kuwa ujanja ujanja wa kula rushwa ulikokufanya kwa miaka kadhaa umekwisha???? Kwa nini usikubali kuwa kila jambo na zama zake na kwamba zama zako zimekwisha?????

Zitto, naongea na wewe achana na Hao vibaraka kina Tundu Lisu..... Ngoja nikwambie, only two rules governs the County inayoendeshwa kwa katiba na sheria yaani sheria zote na Katiba zimeumbwa na kuwa mbili;

Rule #1. Always The President is right na

Rule #2. If you Doubt The President..... Refer Rule #1

Zitto..... Waambie na vibaraka Tundu Lisu na Halima Mdee..... Hivi mpaka leo hamuamini kama Rais wa watanzania ni John Pombe Magufuli.... Au nyie watoto si wa kawaida?????

Rais anazo huruma sana tena sana, na hata jeshi la polisi lonazo huruma sana tena sana..... As kwa mimi, ningewaruhusu mfanye mikutano, then ningewaonyesha Cha mtema kuuni.....

Zitto..... Ule upuuzi na uchochezi uliosema Mbagala.... Ungeweza kuuweka vizuri na kuusema bungeni, sasa wewe bungeni inakiuka sheria, taratibu na kanuni then unakuja kusumbua huku...... Ni sawa na bondia anayeshindwa kupigana ulingoni kisha anakwenda mitaani kupiga kila mtu.... Je huyu bondia ushindi wake uko wapi?????

Kama mna hoja, ilibidi mkae bungeni kwa ustadi na adabu na kufikisha hoja, lakini si kila mnachosema lazima kikubalike.....

Katiba yetu haina referendum.... Mngekuwa wajanja mngetaka muitumie ya Zanzibar kutaka referendum kama watanzania tunataka Bunge live au hatutaki.... Hapo mngeonekana mna akili.....

Lakini sasa ule mtindo wako kila wizara unayochangia lazima useme Bunge live, WASAP, Twitter, Facebook, kwenye engagement yako, na hata ukila ulionyesha udhaifu wa kiwango Cha taka ngumu......

Mwaka 2009 ulitolewa bungeni miezi mitatu tena kwa hoja ya bunge, Na kwa ishu ya Buzwagi ulionekana shujaa..... Ona mwaka huu, unatolewa kwa ishu ya kitoto yaani unalazimisha uwe unaonyeshwa upo wakati upo..... Sasa haupo na Bunge linaendelea... Do you think umejenga?????

Mwisho wa siasa huonekana mapema, na ikiwa hili halitakuwa funzo maalum kwenu, anzeni kuaga kabisa Dodoma..... Lakini jiandaeni maana mnaonekana kama hamridhiki......

Nimeongea na Zitto hao wendawazimu wengine nawahifadhi leo.... Siasa zenu hazina tija, na hata nyie wenyewe hamna tija.....

Tanzania tunahitaji kusonga mbele siyo kila siku maandamano na mikutano..... Ukiona Rais hataki kufanya baadhi ya mambo basi wewe hata usifikirie......

Kama mumeapa kuilinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kiapo Cha Ubunge, then mnataka kuibomoa, ushauri mwepesi ni kuachana na Ubunge, na kuendelea na mambo yenu..... Au hamjui namna ya kuacha Ubunge....???? Chukua karatasi mwandikie Spika.... Kuwa kuanzia leo wewe siyo mbunge tena..... Mbona ni rahisi.... Lakini kwa kuwa mnawaza matumbo yenu tu.... Hilo hata hamlifikirii......

By MTETEZI WA WANYONGE

                      Peter Dafi

#TeamHapaKaziTu......

#TeamMagufuli...........

Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger