Home » » Mikopo kwa wanavyuo wetu na Mtizamo wa UVCCM

Mikopo kwa wanavyuo wetu na Mtizamo wa UVCCM

Written By peterdafi.blogspot.com on Friday, October 11, 2013 | 10:54 AM

SASA NAELEWA
MAANA SUALA LA WANAFUNZI WA VYUO WENYE SIFA ZA KUPATA MKOPO KWA MUJIBU WA VIGEZO VYA BODI,KUKOSA MIKOPO NI SWALA LINALOTAKA MAJIBU YA KINA

SIO LA KUKUBALI KIRAHISI TU
NA HATUWEZI KUKUBALI KIRAHISI MAANA KIFUPI CHAKE NI KUWA SERIKALI IMESHINDWA KUSOMESHA.

NIMERIDHIKA NA MAJIBU YA NAIBU WAZIRI WA ELIMU BWANA PHILIPO MULUGO NA LAZIMA YAFANYIWE KAZI.

KIFUPI ANASEMA;
KWA MUJIBU WA BAJETI YA BUNGE WOTE WENYE SIFA WAMEPEWA MIKOPO BAJETI IMEISHA NA WANACHUO 2000 WENYE SIFA WAMEKOSA.

SASA WAO HAWANA CHA KUFANYA KWA MUJIBU WA TARATIBU LAZIMA WARUDI BUNGENI KUOMBA BUNGE LITAFUTE CHANZO KINGINE CHA MAPATO ILI WALIOSALIA WALIPIWE.

ATA KAMA NIKWAKULIPIA LINE YA SIMU 200 KILA MTU MWENYE UWEZO ALIPE TU NDUGU ZETU WASOME.

1.MASIKINI NA MAYATIMA WASIO NA UWEZO
2.WALIOCHAGUA FANI ZENYE KIPAUMBELE CHA SERIKALI
3.WALIOPATA VYUO VYA KUSOMA

HIVYO NI MIONGONI MWA VIGEZO VYA MSINGI .

SASA TUSISEME AU KUITAKA SERIKALI ILIPE TU

MIMI NAONA TUKUSANYE MAJINA YOTE YA WENYE SIFA
TUWE NA HOJA TWENDE DODOMA TUMWAMBIE WAZIRI MKUU
NA WAZIRI WA ELIMU

UVCCM INAOMBA WANAFUNZI HAO WENYE SIFA MNTAFUTE PAKUZIPATA PESA WALIPIWE.

HII NDIO KAZI KUBWA YA UMOJA WA VIJA WA CCM
NA HAKIKA INAWEZEKANA

UVCCM TUTAENDA PAMOJA DODOMA
ATA KAMA KWA MGUU.

MPAKA BODI WAONGEZEWE FEDHA NA NDUGU ZETU WENYE SIFA WASOME

HATUWEZI KUENDELEA KUWA VIJANA KAMA WA VYAMA VILE VINGINE WAKULALAMIKA TU HAIKUBALIKI.

LETENI MAJINA TUJENGE HOJA
VIONGOZI WAJUU UVCCM TUTAENDA NAO DODOMA.

TUTAFIKA NA TUTASIKILIZWA

TAYARI TUMESHAWASILIANA NA KIONGOZI WA VIJANA WALIOANDAMANA HADI WIZARANI

TUPATE DATA
TWENDENI

NA KWAMUJIBU WA NAIBU WAZIRI WANACHUO 2000 WAMEKOSA MKOPO

SASA KILA MMOJA KWA MWAKA AKIPEWA MILIONI 2 KAMA WATANZANIA CHINI YA SERIKALI TUNATAKIWA KUTAFUTA BILIONI NNE ZA ZIADA

SASA WAZIRI MKUU TUNAKUJA DODOMA BILION NNE TUTAPATEJE
JAMANI TWENDENI

Na Gladness Theonest
PHILIPO MULUGO
"Kasungura kadogo na mkumbuke kuwa mkopo ni kuomba kuna kupata na kukosa...hivyo wale waliokosa na walikuwa na vigezo watafute watu wengine wenye uwezo wawasomeshe kwa mwaka mmoja na unaofuata watume tena maombi," alisema.
Alisema kilio chao amekisikia na leo atazungumza na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuhusiana na malalamiko yao ambapo suala hilo litapelekwa Bungeni ili kujadiliwa.
"Kama Bunge litaamua kupunguza fedha kutoka kwenye bajeti zingine ili kusomesha wanafunzi hao. Bunge litaamua kwani Serikali ina nia nzuri sana kwani hadi sasa imetoa trilioni 1.5, lakini ndugu zenu hawarudishi," alisema.
Alitaja sababu nyingine ya wanafunzi kukosa mikopo ni Serikali kuangalia uhitaji, kwani kuna masomo maalumu walilenga hasa fani zenye upungufu wa wataalamu.
Alitaja fani hizo kuwa ni ualimu, udaktari na wahandisi. Alitaja sababu nyingine za wanafunzi kukosa mikopo hiyo ni waombaji kukosea majina na vitu vingine vidogo vidogo na walipotangaziwa kwenye vyombo vya habari warudi kurekebisha fomu zao hawakufanya hivyo.
Alisema waliokosea kujaza fomu hizo walikuwa 6,000 lakini waliorudi kufanya marekebisho walikuwa ni 3,000 na wengine 2,000 walikuwa na vigezo lakini wamekosa kutokana na sungura kuwa mdogo (bajeti).
Wanafunzi waliokosa mikopo walisema kama wenzao wameweza kupata mikopo kwa asilimia 100 basi waangalie namna ya kugawana ili wote waweze kupata
GAZETI LA MAJIRA
Na Asenga
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger