Home » » CHADEMA YABWAGWA kesi ya Uchaguzi Jimbo la Mlimba.

CHADEMA YABWAGWA kesi ya Uchaguzi Jimbo la Mlimba.

Written By peterdafi.blogspot.com on Thursday, March 10, 2016 | 6:28 AM

CHADEMA YABWAGWA KESI YA UCHAGUZI JIMBO LA MLIMBA

Leo Mchana ilikuwa ni Siku yakusikiliza kesi ya Jimbo la Mlimba ambapo ilikuwa ni Mapingamizi yakisheria yaliyowekwa na Wakili KIBATALA .

Kesi hii ni Dhidi ya Ndg Godwin Kunambi wa Chama Cha Mapinduzi (Aliyekuwa Mgombea) na Bi Suzani Kiwanga Mbunge wa Mlimba kwa Sasa (CHADEMA).

Kesi hii ilifunguliwa Mnamo Tarehe 29/02/2016 na Kesi za Pingamizi la Awali kutoka kwa Mwanasheria wa CDM zilisikilizwa.

Aidha CDM Waliwasilisha na Mwanasheria wao Ndg Peter Kibatala na Mwanasheria Ndg Mtuli toka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Kwa Upande wa Chama Cha Mapinduzi Alisimama Mwanasheria Wao Ndg Godwin Kunambi, Ambae Pia Ndie Haswaa Mlalamikaji wa Kesi hii na Ndie aliyekuwa Mgombea Mwenza Jimbo la Mlimba.

Leo Tarehe 10/03/2016 majira ya Saa nane na Nusu (2:30) Mbele ya Jaji MJULIZI Uamuzi wa Hoja Zao za Mapingamizi Zilitupiliwa Mbali.

Na Kesi ya Msingi itasikilizwa Mala tu baada ya Mahakama Kupanga Tarehe ya Kusikiliza Kesi Hiyo.

Na Peter Dafi

Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger