Home » » Mawaziri Ummy Mwalimu na Mwigulu Nchembe wafungua Machinjio Vingunguti

Mawaziri Ummy Mwalimu na Mwigulu Nchembe wafungua Machinjio Vingunguti

Written By peterdafi.blogspot.com on Monday, April 18, 2016 | 3:33 AM



Mkurugenzi wa manispaa ya ilala Isaya Mgulumi(mwenye miwani) akiwaeleza mawaziri wa wizara ya afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto,Ummy Mwalimu(katikati) na waziri was kilimo na mifugo, Mwigulu Nchemba(kushoto) akiwaelezea hali ya ukarabati wa machinjio hayo


Waziri Mwigulu Nchemba akiongea na Umoja huo na kuwapatia siku tatu ili waendelee na uchinjaji wa ng'ombe walizonazo na baada ya hapo wataendelea na ukarabati wakati huo machinjio ya mazizini yatakua yamekamilisha ukarabati na kufunguliwa


Wanachama wa Umoja wa wafanyabiashara hao waliwasikikiliza mawaziri hao


Mbunge wa jimbo la segerea Bona Kalua,akiongea na wanachama wa Umoja wa Wafanyabiasha wa ng'ombe na mazao yake(UWAMI) kwenye mkutano wa pamoja na mawaziri hao



Mawaziri wakisoma vielelezo vilivyowasilishwa na diwani wa kata hiyo

Mkaguzi toka TFDA dkt. Mwanga Itikija(mwenye shati la pink)akiwaonesha mawaziri hao eneo ambalo lilikua likiuzia nyama kwa reja reja kinyume na kanuni ya afya


Baadhi ya wafanyabiashara wa machinjio hayo wakifuatilia ziara hiyo

Waziri Ummy Mwalimu akiongea na Wanachama wa umoja huo,ambapo.aliwasisitiza kufanya biashara kwa kuzingatia kanuni za afya na kumlinda mlaji hivyo kuwa makini na utunzaji wa mazingira pamoja na mazao wanayoyauza machinjioni hapo


Naibu Meya wa manispaa ya ilaya ambaye ndio Diwani wa kata ya vingunguti Omary Kumbilamoto akiongea kwenye mkutano huo
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. peterdafi - All Rights Reserved
Template Created by Eddie Sucre Published by Bongoclanblog
Proudly powered by Blogger